FURAHA JIJI LA MOMBASA OPERESHENI ZA BANDARI ZIKIREJESHWA PWANI.

  


Waswahili husema, siku njema huonekana asubui. Tarehe 13/9/2022, ndio iliyokua tarehe ya kumwapisha Rais wa tano wa Jamhuri ya Kenya, Daktari William Samoei Ruto na naibu wake Bw. Rigathi Gachagua. Hii ilitokea tu baada ya Wakenya kushiriki kwenye uchaguzi wa Agosti 9,2022 ambapo William Ruto alitangazwa mshindi na Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kupitia kwa Mwenye kiti wake Bw. Wafula Chebukati.

Awali kabla ya uchaguzi, Kaunti ya Mombasa ilitambulika kuwa ngome ya mrengo wa Azimio la Umoja One Kenya unaoongozwa na Raila Odinga. Baadae hii ilidhihirika baada ya uchaguzi, kwani Raila Odinga alizoa kura nyingi zaidi ya mpinzani wake William Ruto. 

Wakazi wa Mombasa wakighadhabishwa na ushindi wake William Ruto, waaliamini kwamba wangesahaulika kwenye serikali Ile, wasijue mpango aliokua nao William Ruto kwao. 

Siku ya Kuapishwa kwake kama Rais wa tano wa Jamhuri ya Kenya, Rais Ruto aliwashangaza wengi kwenye hotuba yake, alipoahidi kurejesha operesheni za bandari Mombasa. 

Ikumbukwe, awali Rais Mstaafu Uhuru Kenyatta alihamisha huduma za bandari toka Mombasa hadi Naivasha. 

Pindu tu baada ya hotuba yake, sherehe, vifijo na nderemo zilishuhudiwa kwenye jiji la Mombasa wakazi wakipongeza hatua ya Rais Ruto kurejesha huduma za bandari Mombasa, jambo ambalo halikusadikika kwao awali. 

Licha ya kutompigia kura na kutoamini alichoweza kuwafanyia wana Mombasa na wa pwani kwa ujumla, pongezi zilimiminika kumshukuru Rias Ruto. 

Pengine mbona wakazi hawa wajawe na furaha kiasi hiki, wakati ni operesheni za bandari tu zimerejeshwa Mombasa? Zipo faida chungu nzima zinazokuja na uwepo wa bandari Mombasa. 

Mojawapo ya faida iletayo bandari kwa wakazi ni nafasi za ajira. Wengi wa watu hupata nafasi za kazi, hivyo kuwawezesha kujikidhi kimaisha. 

Halikadhalika, kulingana na wafanyabiashara wa mapokezi ya mizigo na kuisambaza (CFA), hatua ya Rais Ruto itawawezesha kufufua biashara nyingi ambazo zilififia baada ya operesheni za bandari kuhamishwa kutoka jiji la Mombasa hadi Naivasha. 



Kulingana na Mwenyekiti wa Muungano wa wasambazaji na wamiliki wa Hifadhi za mizigo (Kifwa) Roy Mwanthi, suala la kuhamisha operesheni za bandari ya Mombasa liliathiri biashara huyo ya kupokea mizigo bandarini na kuisafirisha Ile ya magari za kusafirisha mizigo, biashara za hoteli na zingine ndogo ndogo. 

Wafanyibiashara waliotegemea bandari ya Mombasa, walieleza wana Imani kuwa serikali ya Rais Ruto itabadilisha sera nyingi za Bw. Kenyatta, ambazo ziliadhiri uchumi wa jiji la Mombasa na pwani kwa ujumla. 

                                       

                                           By Steve Kinyanjui 



Comments

  1. Sio waswahili ila ni mswahili ambaye ni wewe. Kazi safi ndugu, Naipenda

    ReplyDelete
  2. Ni nzuri...nimefurahishwa na hii kazi

    ReplyDelete
  3. This comment has been removed by the author.

    ReplyDelete

Post a Comment