Posts

Showing posts from November, 2022

TUM YANILETEA UHALISIA WA NDOTO.

Image
  Mara nyingi watoto huwa na maono ya kuwa mtu au kitu fulani katika maisha. Jambo ambalo hukuzwa zaidi na mzazi au hata mwalimu pale shuleni. Ndiposa utamsikia mzazi au mwalimu akimuuliza mtoto angependa kuwa nani awapo mtu mzima. Ni jambo ambalo humwezesha mtoto kufahamu kwamba anao uwezo na nafasi ya kipekee kuwa yeyote atakaye maishani, bora bidii na imani. Kama iwafanyikiavyo watoto wengine, haikua tofauti kwangu. Awali katika umri wangu mdogo, nilitamani sana kuwa daktari, wala si daktari tu bali daktari wa upasuaji. Hili lilitokana na kuwasikiliza watoto wenzangu waliotamani kuwa madaktari, nami nikawaiga. Sikutambua kwamba kila mtu aliumbwa na utofauti wa kipekee na kwamba maishani tungekuwa watu sawa lakini wanaojihusisha na mambo tofauti, nazungumzia wapo wangekua madaktari, walimu, wanahabari na mengineyo. Jambo hili la mimi kuwa daktari liliendelea hadi nilipokuwa katika shule ya upili. Ndipo tulizungumziwa nikiwa kidoto cha pili wakati wa kuchagua masomo manane ambayo ...

JUKUMU LA VIJANA KATIKA KUFUFUA UCHUMI WA NCHI.

Image
  Vijana katika nchi ya Kenya wanalojukumu kubwa mno la kufufua na kukuza  uchumi wa nchi. Wanasema kwamba vijana ndio viongozi wa kesho. Pasipo kuwepo kwa vijana basi taifa lipo kwenye mtego ambao halitoweza kujinasua kesho. Kila uchao, uchumi wa taifa unazidi kuzorota. Bei ya bidhaa inazidi kupanda na kumkandamiza mwananchi wa kawaida. Lakini vijana wana uwezo, ndio wana uwezo wa kubadili hali. Idadi ya vijana ni kubwa sana hapa nchini Kenya. Wapo vijana wanaohitimu kila mwaka kutoka vyuo vikuu. Wapo wanaojihusisha na kazi za  jua kali ambapo wanafanya ufundi mbali mbali, wapo wanaojihusisha na ukulima  pamoja na mengine mengi. Miezi michache iliopita, serikali ya Rais Ruto iliahidi kusambaza mbolea kwa wakulima nchini ili wakuze chakula na ili baadae uchumi wa taifa uweze kurejea katika Hali ya awali. Vijana wanaojihusisha na ukulima walifaidika na mradi huu ambapo baadae serikali itawanunulia bidhaa zao na kupitia mazoa watakayo kua wamekuza, bei za bidhaa zitawe...