Posts

Showing posts from October, 2022

ATHARI ZA MABADILIKO YA HALI YA HEWA.

Image
  Mabadiliko ya Hali ya hewa yameshuhudiwa katika nchi tofauti Duniani ambapo mimea, wanyama na binadamu wameadhirika na wengine hata kufariki dunia. Hata hivyo, Kenya haijasazwa, kwani tumeshuhudia baadhi ya maeneo nchini yakiadhirika kwa ukame ambapo mimea imenyauka, wanyama nao sawia na binadamu wakidhoofika na kufariki, yote kwaajili ya ukosefu wa maji/mvua. Ni juzi tu ambapo takriban Kaunti thelathini zimeripotiwa kuadhirika kwa ukame na kuwa serikali inajitahidi kuhakikisha kwamba maeneo haya yanasaidiwa kwa kupewa msaada wa  chakula. Hii ni baadhi ya madhara yaletwayo na mabadiliko ya Hali ya hewa. Ukosefu wa mvua husebabisha ukame ambapo viumbe wengi, wanyama kwa binadamu sawia na mimea huadhirika pakubwa.  Waswahili husema kwamba maji ni uhai, hii imedhihirika dhahiri siku chache, wakati wakazi wa Kaunti ya Baringo walionekana wakichimba mto uliokauka ili angalau wapate tone la maji. Baya zaidi ni kwamba maji waliotafuta kwa udi na uvumba yalikua ni maji machafu ...

FURAHA JIJI LA MOMBASA OPERESHENI ZA BANDARI ZIKIREJESHWA PWANI.

Image
   Waswahili husema, siku njema huonekana asubui. Tarehe 13/9/2022, ndio iliyokua tarehe ya kumwapisha Rais wa tano wa Jamhuri ya Kenya, Daktari William Samoei Ruto na naibu wake Bw. Rigathi Gachagua. Hii ilitokea tu baada ya Wakenya kushiriki kwenye uchaguzi wa Agosti 9,2022 ambapo William Ruto alitangazwa mshindi na Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) kupitia kwa Mwenye kiti wake Bw. Wafula Chebukati. Awali kabla ya uchaguzi, Kaunti ya Mombasa ilitambulika kuwa ngome ya mrengo wa Azimio la Umoja One Kenya unaoongozwa na Raila Odinga. Baadae hii ilidhihirika baada ya uchaguzi, kwani Raila Odinga alizoa kura nyingi zaidi ya mpinzani wake William Ruto.  Wakazi wa Mombasa wakighadhabishwa na ushindi wake William Ruto, waaliamini kwamba wangesahaulika kwenye serikali Ile, wasijue mpango aliokua nao William Ruto kwao.  Siku ya Kuapishwa kwake kama Rais wa tano wa Jamhuri ya Kenya, Rais Ruto aliwashangaza wengi kwenye hotuba yake, alipoahidi kurejesha operesheni za ban...

CHOZI LA PENZI.

Image
  Jina penzi litajwapo, kila mmoja hupiga taswira ya kile alichopitia ndani yake. Wengi wanapenda kwa maana hawajatendwa, wengine wanahofu, yasirejelee yaliowakuta awali na bado wapo wasio na Imani tena, kwa maana walishatendwa, wakalizwa, wakajeruhiwa na kuachiwa majeraha yasiyopona, na kwa wale waliopona, waliachwa na alama, alama ziishizo kuwapa kumbukumbu za awali milele. Waswahili wanasema, yaliyopita si ndwele tugange yajayo. Lakini, watayaganga vipi wakati nyoyo zilishalemaa? Wakati picha za akili, daima zinawapa kumbukumbu ya kusalitiwa, kudharauliwa na kutodhaminiwa na watu walio ishi kesema 'nakupenda' na kamwe sijapata kama wewe?  Inauma. Lakini, hivi Mapenzi ninini? Mbona upende leo na kesho uchukie? Mbona usifu leo na kesho ukashifu? Mbona? Ama kwakweli, huu ndio mtindo wa mapenzi unaotumika na kupatikana ndani ya vyuo vikuu. Sisemi kwamba nje watu wanapendana asilimia 100, la hasha! Tumeshuhudia nyingi za ndoa zikisambaratika, kisa na maana 'mpango wa kando...